Wednesday

JK NA MAMA SALMA WASALIMIANA NA DAVID BEKHAM




Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakisalimiana na mchezaji soka nyota wa Uingereza anayechezea Los angeles Galaxy ya Marekani,   David Beckham,  walipokutana uwanja wa ndege wa Heathrow jijini London Jumatano, muda mfupi kabla ya Rais Kikwete na Mama Salma kuelekea Washington DC kuhudhuria mkutano wa G8 kwa mwaliko wa Rais Barak Obama wa Marekani. Bekham ameonesha nia ya kutembelea Tanzania kama mtalii siku za karibuni na Rais Kikwete amemkaribisha kwa mikono miwili, akimhakikishia kwamba licha ya kuwa na mashabiki wengi ambao watafurahi kumuona pia atafurahia vivutio kibao vya kitalii.

CHARLES TAYLOR KITANZINI

  •  Asema mashahidi walinunuliwa

Rais wa zamani wa Liberia Charles Taylor

Rais wa zamani wa Liberia Charles Taylor anayetuhumiwa kwa makosa ya kivita amewashambulia waendesha mashtaka kuwa waliwalipa mashahidi wa upande wa mashtaka ili wamkandamize.
Taylor ambaye alikutwa na hatia mwezi uliopita alisema hayo wakati akitoa maelezo kwenye mahakama ya Kimataifa ya makosa ya Jinai ya The Hague.
Hiyo ni nafasi yake ya mwisho ya kujieleza katika mahakama hiyo kabla ya kusomewa hukumu baadae mwezi huu.
Taylor alipatikana na hatia ya kuwasaidia waasi nchini Sierra Leone wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe ambapo pia anaelezwa alisaidia kuendesha mipango ya mauji.
Akitoa maelezo yake Taylor amesema fedha imechukua nafasi katika kesi yake.
"Mashahidi wamelipwa , wamelazimishwa na kwa wakati fulani walitishiwa na waendesha mashtaka kama wasingetoa ushahidi unaonikandamiza", alisema.
Amesema yeye mara zote alikuwa akilaani maauaji popote duniani na aliwahurumia waathirika wa mauaji hayo.
Nje ya mahakama Taylor mara zote amekuwa akipinga makosa yote 11 yanayomkabili huku akisisitiza kuwa hana hatia yoyote.

MAPINDUZI MAKUBWA KUTOKA CHADEMA?

  • Shibuda atangaza kugombea Uraisi 2015 akiwa CHADEMA


BAADA ya mwaka 2005 kuwania urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kubwagwa katika hatua za awali, Mbunge wa Maswa Mashariki, John Shibuda, kwa mara nyingine ametangaza kuwania nafasi hiyo kwa tiketi ya Chadema mwaka 2015.
Shibuda alitangaza azma yake hiyo juzi mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kwenye semina iliyofanyika Dodoma katika ukumbi wa Nec ya CCM iliyojadili hali ya utawala bora nchini iliyotolewa na taasisi inayotathmini utawala bora Afrika (APRM).
Shibuda ni mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo anayewakilisha vyama vya upinzani.
"Nakupa pole, kazi ya urais ni ngumu sana, bila shaka utakumbuka kuwa nami nilitaka kuwa mbadala wako, hata hivyo naamini utakuwa meneja wangu wa kampeni za urais mwaka 2015," alisema Shibuda.
Huku wajumbe wa NEC wakishangalia, Rais Kikwete alimwuliza: "unataka urais kupitia chama gani?" Shibuda akajibu kwa kujiamini: "Kupitia Chadema, huku niliko sasa”.
Kauli ya Shibuda imekuja wakati kukiwa na minong'ono ya baadhi ya wanasiasa wazito ndani ya chama hicho kutaka kuwania nafasi hiyo.
Wanasiasa wanaotajwa kutaka kwa udi na uvumba kuwania nafasi hiyo kupitia Chadema, ni Mwenyekiti wa Chama hicho, Mbunge wa Hai Freeman Mbowe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe na Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa ambaye aliwania mwaka 2010.
Huku akishangiliwa na wajumbe wa NEC Shibuda alisema kwa kuwa mwaka 2005 aliomba ridhaa ya CCM kugombea urais akakosa nafasi hiyo alimwomba Rais Kikwete awe mpiga debe wake na kuamini kuwa kwa kazi nzuri aliyofanya nchini kwa kipindi cha miaka aliyokaa madarakani, akimpigia debe bila shaka atafanikiwa.
Kikwete akamwuliza anataka ampigie debe kupitia chama gani? Shibuda akajibu “kupitia Chadema,” wajumbe wa NEC wakamshangilia kwa nderemo na vigelegele.

Shibuda pia alizungumzia nafasi ya CCM katika siasa ya Tanzania, na kusisitiza kuwa hivi sasa hakuna mbadala wa CCM katika kuongoza nchi.
Alisisitiza kuwa CCM imejijenga kimfumo kuanzia ngazi ya juu mpaka mashinani, jambo ambalo linarahisisha utoaji haki kuanzia chini mpaka juu.
Mbunge huyo, alisisitiza kuwa tatizo ndani ya CCM ni baadhi ya viongozi kuwa wabinafsi ambao aliwafananisha na kunguru wasiofugika, kwa kutofuata miiko na maadili ya chama na badala yake kuwa sehemu ya watu wanaoharibu chama hicho.
Hata hivyo, alisema pamoja na yote, bado nafasi ya CCM kuendelea kuongoza Dola ni kubwa, kwani mpaka sasa vyama vya siasa vya upinzani, bado havijawa na uwezo wa kutekeleza chochote zaidi ya CCM.

Q-CHIEF AVUNJA UKIMYA


Msanii wa kizai kipya, "Q-Chief" ametoa kibao kipya kinachokwenda kwa jina la "UMGENIUMIZA" ambapo unatarajiwa kubamba kila kona kitaani kutokana na maandalizi ya kutosha yaliyokuwepo hadi kuachiwa kwa ngoma hiyo babkubwa. Unaweza ukajiuliza sana kwanini Q-Chief alikuwa kimya kwa muda mrefu kidogo kabla ya kuanza kuachia “mabomu” takribani tangu mwaka jana hivi.In short ni kwamba Chilla anaweza.....Ana kipaji na pengine kama alivyowahi kusema katika mahojiano na media miaka ya nyuma kidogo, kuwa yeye ni tajiri wa sauti. Isiwe kesi.....kudownload songi hilo fuata linki hii hapaa  (BongoCelebrity)

ATC YAPATA NDEGE MBADALA: HILI NALO LINAHITAJI KEKI NA MASHADA YA MAUA?

Yapo mambo ambayo hata unapotaka kuyakalia kimya tu inakuwa shida kidogo.Juzi,Shirika La Ndege Tanzania(ATC) limepata ndege mbadala(nasema mbadala badala ya mpya kwa makusudi).Ndege hii imekodishwa...Je ni kweli kuwa Uwezo wa kununua bado hatuna?.Cha kusikitisha zaidi ni kwamba tunavishana mataji kujipongeza kwa kufanikiwa kukodi ndege moja ya abiria!!!!????
Pamoja na hayo,kwetu sisi yaelekea kuwa na ndege ya kukodisha ni mafanikio makubwa sana.Yanastahili makofi,vigelegele na keki.Kweli??
 
Wafanyakazi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakishuka katika ndege mpya aina ya Boeing 737-500 iliyokodishwa na shirika hilo yenye uwezo wa kubeba abiria 108. Ndege hiyo itaanza kuruka baada ya wiki moja.
 
Kaimu Mkurugenzi na Mwenyekiti Mtendaji wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) Paul Chizi akiongea na waandishi wa habari mara bada ya kuwasili kwa ndege mpya aina ya Boeing 737-500 iliyokodishwa na shirika hilo yenye uwezo wa kubeba abiria 108.
 
Wafanyakazi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakikata keki kusherekea ujio wa ndege ndege mpya aina ya Boeing 737-500. Wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi na Mwenyekiti Mtendaji wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL ) Paul Chizi
GOD SAVE US!
Picha na maelezo ya picha kwa hisani ya G.Sengo

Saturday

SAFARI YA BONGO FLEVA HIYOOO KUNAKO MITAANI

  • Awa mfano wa kuigwa kwa kusaidia yatima

    • Ni wasanii wangapi wanagonga kopi za kutosha na shoo kibao lakini husahau walikotoka? Bongo Artists take this aaand ACT. 

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond, baada ya kuwa na mafanikio katika muziki wake ameanzisha mpango wa kusaidia jamii yake kama sehemu ya shukrani kutokana na mafanikio hayo, ukizingatia jamii kwa kiasi kikubwa ndiyo inayomsapoti.
hapa yeye mwenyewe (kulia) akitoa msaada wa vyakula na vitu vingine kwenye kituo cha kulea watoto yatima cha Maunga kilichopo Kinondoni Hananasif jijini Dar es Salaam.

MISS IFM 2012 KUTAKUWA NA JIPYA USIKU WA LEO??



Wakati harakati za kumsaka mrembo atakayekabidhiwa taji la Miss IFM 2012 zikiwa zinaelekea ukingoni, mashabiki na wapenzi wa industry hii ya urembo wameonekana kujawa na shauku ya kutaka kufahamu ni kipi hasa kitakuwa kipya ama cha kipekee katika mashindano haya 
 Mtanange wa kumtafuta mrembo atakeiwakilisha IFM katika mashindano ya mrembo wa vyuo vikuu unaendelea na tayari mabinti wameiva kama mnavyowaona.
 ...hapa ni maelezo kutoka kwa mwalimu kuja kwa washiriki na mpiga picha pia...
 Hapo VP?
Warembo watakaoshiriki shindano la Redds Miss IFM 2012 wakiwa kwenye pozi la picha ya pamoja kwenye mazoezi yananyika kwenye ukumbi wa Break Point Posta mpya jijini Dar Es Salaam kwenye maandalizi ya fainali itakayofanyika kwenye fukwe ya Cine Club jijini Dar Es Salaam usiku wa jumamosi ya 12/05/2012

BAADA YA KANUMBA, KIFO SASA CHAMUANDAMA JB



MCHEZA filamu anayetamba kwenye ‘game,’ Jacob Steven ‘JB’ (pichani) hivi karibuni alinusurika kuuawa na majambazi waliovamia Pub ya msanii mwenzake, Aunt Ezekiel iliyopo eneo liitwalo Gereji Mwananyamala jijini Dar.
Akizungumza na Mpekuzi wetu, JB alisema kuwa baada ya majambazi hao kuvamia katika pub hiyo saa 5.30 usiku, hakuwastukia kama walikuwa wahalifu bali alidhani ni wateja wa kawaida.


“Mimi sikuwashitukia kama wale watu walikuwa majambazi, ila baada ya kutoa bastola na kutuamuru tulale chini na tutoe kila kitu nikajua kimenuka, nikatimua mbio ambazo sijawahi kukimbia licha ya mwili wangu huu,” alisema JB.


Aliongeza kuwa, wakati akitimua mbio aliwasikia watu wakimuaru asimame lakini hakutii hadi alipofika Kituo cha daladala cha Komakoma ndipo alisimama na kumshukuru Mungu kwa kumnusuru na kifo.

Mei 7, mwaka huu usiku, majambazi kadhaa waliivamia pub ya Aunt Ezekiel na kufanikiwa kupora fedha na kumjeruhi mkononi na mgongoni kwa risasi kijana mmoja aitwaye Musa mkazi wa Sinza.

Nyeti za mwanaume zanasa ndani ya uke wa mke wa mtu Nairobi

Image of Nyeti za mwanaume zimenasa ndani ya uke wa mke wa mtu Nairobi [Video]

Wakati wa mchana katika kijiji cha TASSIA, EMBAKASI NAIROBI jamaa mmoja amekutwa akiwa AMEKWAMA yani mwili wake na umenasa na kukataa kuachiana na mwili wa MKE WA MTU walipokuwa wanajiburudisha.


JAMAA mwenyewe anadaiwa kuwa wa jamii ya WAKISII na mke wa mtu ana asili ya jamii ya WAKAMBA, ambapo inasemekana baada ya stori kuendelea sana kwamba jamaa anaiba mke wa mtu, MUME ilibidi aende kwa MGANGA kumfunga MKE WAKE ili asifanye mapenzi nje ya NDOA na akifanya hivyo ATAKWAMA, yani kukwamba wana maanisha jamaa yeyote atakae ingia kwenye mtego mwili wake hautoachana na mwili wa mwanamke huyo, itashikana na aibu iwakute

REVOLUTION TIME KWENYE GAME LA BONGO YAWADIA

Studio mpya - "DIGITAL VIBES" - kufunguliwa Morogoro maeneo ya Masika

Thursday

WANAFUNZI WANASOMA KWA KUGEUZIANA MIGONGO RUVUMA

WANAFUNZI 201 kuanzia darasa la tatu hadi la sita  katika shule ya msingi Kidugalo kata ya Rwinga wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma wanasoma katika vyumba viwili vya madarasa kwa kugeuziana migongo hali ambayo inachangia kushusha taaluma katika shule hiyo.
Wanafunzi wa darasa la tatu na la nne katika shule ya msingi Kidugalo kata ya Rwinga Namtumbo mjini mkoani Ruvuma wakisoma katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Owini Mpangala alibainisha kuwa  wanafunzi 51 wa darasa la tatu na wanafunzi 56 wa darasa la nne wanasoma katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo na wanafunzi 62 wa darasa la tano na wanafunzi 32 wa darasa la sita wanasoma katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo.
“Madarasa mawili kusomea katika chumba kimoja kunasababisha kila darasa kufundishwa vipindi vinne tu kati ya vipindi nane vinavyotakiwa kufundishwa kwa siku,walimu wawili hawawezi kuingia kwa wakati mmoja kufundisha kwenye chumba kimoja,vipindi vinne vinapotea  darasa halifundishiki’’,alisisitiza.
Kwa mujibu wa mwalimu Mpangala shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2007 yenye wanafunzi 453 ina vyumba vinne tu vya madarasa kati ya mahitaji ya vyumba nane na kwamba shule hiyo haina ofisi ya walimu hali ambayo inasababisha mwalimu mkuu na walimu kutumia ofisi moja ambayo hata hivyo haitoshi kutokana na idadi ya walimu 13 waliopo katika shule hiyo.
Kutokana na hali hiyo baadhi ya walimu wanakaa nje ya ofisi wakati wa kiangazi huku wakiendelea kufanyakazi za kusahihisha madaftari ya wanafunzi wakipigwa na jua hali ambayo inaleta kero kubwa kwa walimu na wanafunzi.
Mkuu wa shule hiyo alisema amechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na matatizo hayo ikiwa ni pamoja na kuyapeleka katika kamati ya shule na Baraza la madiwani ambayo wameahidi katika msimu ujao wa fedha wanatarajia kulipatia kipaumbele hasa kero ya upungufu wa vyumba vya madarasa,samani na ofisi ya walimu.
“Hapa kwangu uongozi wa serikali ya kijiji umekataa kujenga vibanda vya nyasi kama ilivyo katika shule nyingine kwa madai kuwa hapa ni mjini hawawezi kujenga vibanda vya nyasi ni aibu,wamefyatua tofali zipo kwenye tanuri’’,alisema.
Baadhi ya walimu wanaofundisha katika shule hiyo wamesema wanatamani kuacha kazi au kuhama katika shule hiyo kutokana na changamoto nyingi ambazo hazijapatiwa ufumbuzi kwa muda mrefu na kuchangia kushusha elimu katika shule hiyo ambayo ipo mjini.
Mratibu elimu kata ya Rwinga Thomas Komba amekiri shule za msingi katika kata yake inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo shule ya msingi Kidugalo ambapo hivi sasa uhamasishaji unafanyika ili kumaliza kero ya upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa.
Baadhi ya walimu katika shule ya msingi Kidugalo wakisahihisha madaftari ya wanafunzi nje baada ya shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2007 kukosa ofisi ya walimu

Aliongeza kuwa wananchi wa eneo la Kidugalo mwaka jana wamefyatua na kuchoma tofali kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na kwamba hivi sasa kinachosubiriwa ni nguvu toka serikalini kutoa vifaa vya kiwandani ili kuweza kufanikisha kupunguza kero hiyo ya muda mrefu.
Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo ina shule za msingi 107 kati ya hizo shule 105 zinamilikiwa na serikali na shule mbili ni za watu binafsi na mashirika ya dini.
Imeandaliwa na Albano Midelo,Namtumbo

Sunday

MASTAA 7 NDANI YA BIG BROTHER 2012.


lADY MAY (25) NAMIBIA.
PREZZO (32) KENYA.
BARBZ (34) SOUTH AFRICA.
ROCK (27) ZIMBABWE.
MAMPI (25) ZAMBIA.

DKB (26) GHANA.

GOLDIE (28) NIGERIA.photos by Global Publishers.

MIMBA YA LULU YAZUA UTATA

Utata kama Elizabeth Michael ‘Lulu’, (pichani)  ana mimba au la, umetatuliwa baada ya mwanamitindo maarufu Bongo anayefahamika kwa jina moja la Martin kutoboa siri kuwa ni kweli staa huyo ana mimba ya miezi mitatu, Risasi Jumamosi linafunguka.
Akizungumza na mwandishi wetu, Martin ambaye ni rafiki wa karibu wa Lulu anayesota rumande Segerea, Dar akiwa mshukiwa wa kwanza wa kifo cha Steven Kanumba, alisema kwa hesabu zake tangu msichana huyo aliponasa ni takribani miezi 3 sasa.
WALIJARIBU KUICHOROPOA MARA KADHAA
Jamaa huyo alifunguka kuwa baada ya Lulu kushtuka kuwa ni mjamzito alimweleza marehemu Kanumba ambapo kwa pamoja walijaribu kuichoropoa mimba hiyo lakini ikasema “sitaki” (ikashindikana).

Aliendelea kudai kuwa, baada ya mpango huo kufeli waliamua kuiacha hadi Lulu alipokumbana na dhahama ya kukaa nyuma ya nondo hadi leo.


“Yeye (Lulu) na Kanumba walijaribu mara kadhaa kuitoa lakini ikashindikana.”alisema mwanamitindo huyo.
 NDIYO CHANZO CHA ‘SHESHE’ LAO
Jamaa aliweka wazi kuwa ‘sheshe’ kubwa kati ya Lulu na marehemu Kanumba lilihusiana na mimba hiyo.
 “Kanumba alikuwa akitaka Lulu akatoe mzigo huo, lakini Kalulu Kadogo (Lulu) alikataa katakata,” alisema na kuongeza:
“Aisee ilikuwa ni ishu ya siri sana.”
TUJIKUMBUSHE
Madai ya Lulu kuwa mjamzito yaliripotiwa kwa mara ya kwanza wiki iliyopita na gazeti ndugu la hili la Amani ambapo ilielezwa kuwa mbali na kitumbo kumtoka pia, alikuwa akichagua aina ya vyakula.

KILI AWARDS YAENDELEZA SHANGWE MWANZA


Monday

JK AIONGOZA KAMATI KUU WHITE HOUSE




Rais Jakaya Kikwete (wa kwanza kulia) akiongoza kikao cha kamati kuu ya CCM leo Ikulu. Picha na Ikulu.

JK AWASILI TANGA KUSHEHEREKEA MEI MOSI KESHO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na mamia ya wakaazi wa jiji la Tanga leo April 30, 2012 baada ya kuwasili kuwa mgeni rasmi kesho katika sherehe za Mei Mosi



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya mamia ya wakaazi wa jiji la Tanga leo April 30, 2012 baada ya kuwasili kuwa mgeni rasmi kesho katika sherehe za Mei Mosi



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa ka furaha na Katibu Mkuu Shirikisho la Vyama vya Wafanyaakzi Tanzania (TUCTA) Bw Nicholaus Mgaya  leo April 30, 2012 baada ya kuwasili kuwa mgeni rasmi kesho katika sherehe za Mei Mosi

Sunday

Rais wa Malawi amfuta kazi hasimu wake

Rais mpya wa Malawi Joyce Banda amemfuta kazi Waziri wa mambo ya nje Peter Mutharika, kakake Marehemu Rais Bingu Wa Mutharika aliyefariki dunia mwezi huu.

Mutharika alitarajiwa kurithi Marehemu Kakake katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2014 ambapo Bingu Wa Mutharika alitarajiwa kustaafu.
Mabadiliko ya baraza la mawaziri yametokea siku chache baada ya maziko ya Rais huyo mapema wiki hii. Bi. Banda amekuwa Makamu wa Rais tangu mwaka 2009 lakini akatofautiana na Wa Mutharika na kuwa mksoaji wake mkubwa.
Kufuatia kifo cha Rais huyo kulizuka wasi wasi kwamba wandani wake wangejaribu kuzuia ukabidhi wa madaraka kwa Bi. Banda ambaye alikuwa na chama chake cha kisiasa.
Miongoni mwa Mawaziri wapya ni Austin Atupele Muluzi, mwanawe Rais wa zamani Bakili Muluzi aliyeteuliwa Waziri wa mipango na ustawi.Wengi waliotimuliwa na waliokuwa wandani wa Bingu Wa Mutharika.

Kanisa lashambuliwa Nairobi

29 Aprili, 2012 - Saa 08:51 GMT

Mlipuko kwenye kanisa mjini Nairobi, Kenya, umeuwa mtu mmoja na kujeruhi wengine 10.
Polisi wanasema guruneti lilirushwa kwenye kanisa la God's House of Miracle kwenye mtaa wa Ngara, wakati wa ibada ya asubuhi.

Daktari mmoja katika Guru Nanak Hospital mjini Nairobi, ambako ndiko majeruhi walikopelekwa, aliwaelezea waandishi wa habari majeruhi aliowaona:

"Tumepokea majeruhi 7, mwanamke mmoja aliumia vibaya kwenye mguu wa kushoto, ambao umevunjika mahala kadha.

Mwanamme mmoja alikuwa na majaraha kadha kwenye nyama na tunafikiri amevunja mifupa piya; labda tukimfanyia x-ray tutatambua.

Kuna mama mmoja aliyevunja kidogo kisuguru cha mguu wa kushoto, na wengineo wamepata mikwaruzo-kwaruzo na kujikata-kata."

Kumetokea mashambulio kadha ya maguruneti nchini Kenya tangu mwaka jana pale serikali ilipotuma wanajeshi Somalia kupambana na wapiganaji wa Kiislamu, Al-Shabaab.

Search This Blog