Sunday

NIMEIPATA, PICHA NA VIDEO YA MAGOLI YOTE KATI YA HANNOVER 96 NA MAN U UJERUMANI AUG 11 2012! CHEK WALICHOFANYA KAGAWA NA ROONEY!



.


Wafungaji ni Chicharito, Kagawa na Rooney aliefunga mawili.. mechi ilikua kali sana! hiyo video hapo chini ndio ushahidi pekee wa magoli ya timu zote mbili… ichek alafu uniambie!



           

AY NDIO ANAKWENDA TENA MAREKANI, KINACHOMPELEKA NDIO HIKI ALICHOKISEMA.

Ay, Lamyia na Hemdee…. 

Kama haufahamu, kolabo ya kwanza ambayo haikutoka ya Ay na Sean Kingston ndio ilimfanya Ay kuombwa kolabo na Lil Romeo na Lamyia Good baada ya kuisikia studio huko Marekani.

Naona siku zinahesabika na zimebaki chache kwa ajili ya Ay kuchukua pipa moja kwa moja mpaka Los Angeles Marekani kwa ajili ya kufanya ile project kubwa ambayo kila alieisikia taarifa yake zaidi ya mwaka mmoja uliopita amekua na hamasa ya kusikia nini kinaendelea.

Mwimbaji Staa Sean Kingston alipokuja bongo mwaka juzi alitangaza kupitia XXL ya CLOUDS FM kwamba yuko tayari kufanya kolabo na Mtanzania Ay ambapo siku kadhaa mbele, Ay alinisikilizisha wimbo wake aliorekodi Marekani ambayo ndio kolabo na Sean Kingston.

Ulipita muda wa ukimya kidogo baada ya Ay kurekodi audio ya kolabo ya kwanza na Kingston ambayo ndio alinisikilizisha, ukimya ulifata baada ya hapo lakini kumbe Ay alikua anavuta subira na kuongeza uvumilivu kutokana na ratiba nzito ya Kingston ambae alikubali kufanya nae kolabo bure, wakati Jose Chameleone wa Uganda kwenye kolabo aliyoahidiwa na Sean Kingston ameambiwa atailipia USD elfu 30 ambazo ni zaidi ya milioni 45 za kibongo.

Ay amesema “Marekani nakwenda September 2012 kufanya kolabo na Tyga wa Cash Money pamoja na video na Sean Kingston, hizi kazi zinahitaji hela lazima uwe unajipanga kwelikweli yani ukienda unafanya kazi unamaliza unarudi zako”
                                            Los Angeles.


Millard Ayo alipomuuliza kama amekamilisha kolabo kwa upande wa audio na Sean Kingston, Ay amejibu “unajua mimi na Sean tumerekodi nyimbo mbili, tulirekodi nyimbo ya kwanza ambayo wewe ndio uliisikia nakumbuka baada ya hapo walipoona ‘party zone’ akasema eeehhhhh uko serious eeh? ile ya kwanza tuachane nayo ngoja tufanye kitu kingine kizuri zaidi na kusema kweli ukisikiliza wimbo wa kwanza na wimbo wa pili, wa pili ni mzuri zaidi na ndio ambao tunashoot”

Ambwene amesema kwa sasa hawezi kutaja jina la hiyo new single ya pili lakini video itafanyika Las Angeles, producer ni yule yule alierekodi ‘speak with your body’ na ndio anaefanya kazi za Sean Kingston, za Soulja Boy, ni injinia wa Akon na Lady Gaga pia.

Video ya ‘party zone’ ya Ay iliyomshawishi Sean kubadili maamuzi ilipelekwa kwake june 2012 na meneja wa Ay ambae ni Hemdee mwenye mchanganyiko wa Mganda na Mmarekani ambapo ilimfanya Sean Kingston kurekodi hiyo kolabo ya pili mwishoni mwa mwezi wa sita.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI AUG 12 NA STORI ZILIZO-MAKE HEADLINE KITAA


















































Thursday

VIWANGO VIPYA VA FIFA NDIO HIVI, SPAIN BADO INAONGOZA… CHEK TANZANIA ILIPO, MOJA TU YA AFRIKA NDIO IPO 20 BORA.!




.

Timu ya Taifa ya Spain imeendelea kukalia kiti cha uongozi wa ubora wa soka kwa mujibu wa viwango vya FIFA. Mabingwa ha wa dunia na ulaya wameshikilia uongozi huo wakiwa na pointi 1605, nafasi ya pili imekamatwa na Ujerumani, England wameendelea kupanda ubora kwenye rank hizo za FIFA bada ya mwezi uliopita kushika nafasi ya nne.

Brazil mabingwa wa mara tano wa dunia wameendelea kuweka rekodi, baada ya kushika nafasi ya chini zaidi katika historia yake, wakikamata nafasi 13, ikiwa ni mara ya kwanza kushuka kwa namana hiyo.

Ivory coast ndio pekee ya kiafrika kuwemo ndani ya 20 bora, wakishika nafasi ya 16. Timu ya taifa ya Tanzania imeshuka kwa nafasi moja kutoka nafasi ya 127 mpaka 128. (imeandikwa na mwandishi maarufu wa habari za michezo Shaffih Dauda wa Clouds Fm)


.

VIDEO YA GAME YA MANCHESTER UNITED NA BARCELONA AUG 8 2012 ILIVYOKUA NA MATOKEO.

 

Tuesday

Strike will not bar teachers from census, clarifies govt



Kassim Majaliwa

The government has said that the recent strike will not disqualify teachers from supervising the August 26 Tanzania Population and Housing Census.

This was revealed yesterday by deputy minister Prime Minister’s Officer, Regional Administration and Local government, Kassim Majaliwa when asked to clarify claims that some government authorities were planning to bar teachers from supervising the census exercise.


Through a telephone interview with The Guardian yesterday, Majaliwa confirmed that teachers will participate fully in the processes as planned.

“The government has no plans to bar teachers from supervising the census, nor have they planned so,” said Majaliwa.
The deputy minister said teachers’ demands cannot be linked to the census process because they are two different things. “Teachers’ interests are well known. What they were demanding is for the government to increase their salaries,” he stressed.

He added that because the census was a special activity and will be conducted throughout the country, the government has decided to close schools so that teachers can help the government in carrying out the exercise. 
Majaliwa called upon teachers to support the government during the census. “We have not said only teachers will supervise census, but there are vacancies for those who are interested,” he clarified.

The deputy minister said however that there are many graduates in villages who can be of help in supervising the exercise.
“They are going to collaborate with teachers in monitoring the census,” said Majaliwa.

He said it was the task of regional and district census coordinators to get qualified supervisors of the census.
SOURCE: THE GUARDIAN

KITU KIPYA NDANI YA BONGO MUVI.........ARE YOU REEAADY?????





Ni filamu mpya kabisa inaitwa NZOWA ambapo ndani kuna Mzee MASHAKA wa kaole, NATASHA, WASTARA, SAJUKI, TINO, MUHOGO MCHUNGU, DUDE pamoja na wengineo na ni filamu inayozungumzia maisha...


                                           UNAIONAJE COVER!!!???

SINTAH AOMBA MUMPE SIFA YAKE YA USOMI

 daah kweli msomi, mpaka nasinzia kwa point kichwani
shurti kwa mifano chezeya International Relations and Diplomacy


heeeee nikitoa lecture,miniwache mie



Lolest huyu huyu J wake Lo,jeshi la mtu mmoja daah kweli Mungu akikuandikia amekuandikia hata kama binaadam wazibe vipi wanachemka,fitina yako bahati yangu. Mungu alishapanga
kuwa nitakuwaje so utachelewesha tuu lakini lazime litimie, nikiwa kama mgeni rasmi na wengineo nilipewa muda wa kuongea heeee kama wangekuwa wakina mwanafulenge wangejikojolea maana baada ya speech ni maswali tuu,mtu ana nyoosha kidole na nina jibu hapo kwa hapo, sikwenda hata na karatasi point zilitoka kichwani according na maswali, halafu sio maswali ya huku ktk web,maswali kuhusu umoja wa mataifa na mengine ya economy haya wee asha ngedere ungejibu jamani??nipeni sifa yangu tafadhali.
watu waliokuwepo pale waulizeni kila siku nawaambia KNOWLEDGE IS POWER.
muniwachagee basi its my time ku shine ki diplomat ,,,, sio kwamba ninajisifu ninasema kweli
for more pics nitaandika blog ya kuangalia uzinduz wa kitabu cha siri ya mafanikio.
story na sintah.com

KUHUSU MGOGORO WA MPAKA NA MALAWI, HII NDIO KAULI MPYA YA TANZANIA.

Straight kutoka bungeni Dodoma kuhusu ishu ya mpaka wa Malawi na Tanzania ni kwamba waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe amesema Malawi wanadai kwamba mpaka wa Tanzania na wao kwenye ziwa Nyasa unapita Pwani hivyo ziwa lote kutoka kwenye mpaka wa Malawi na Mozambique hadi Kyela ni mali ya Malawi.

Amesema “serikali yetu ilipata habari za kuaminika kupitia shirika la TPDC kuwa eneo lote la ziwa Nyasa kaskazini mwa Msumbiji limegawanywa kwenye vitalu na kwamba serikali ya Malawi imevitoa vitalu hivyo kwa kampuni ya utafiti wa mafuta na gesi”

“Makampuni hayo yaliomba kibali cha kuruhusu ndege za utafiti ziwani humu ombi ambalo jeshi la Wananchi wa Tanzania lilikataa, pamoja na katazo hilo serikali yetu ilipata ushahidi kwamba ndege ndogo za utafiti zenye uwezo wa kutua majini na ufukweni zinazokadiriwa kuwa tano zilionekana zikivinjari na kutua katika ziwa Nyasa upande wa Tanzania na kwenye ufukwe wake January 29 na July 2 2012″ – Bernard Membe

“Serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania inathamini sana uhusiano mzuri uliopo baina ya nchi mbili na ina dhamira ya kudumisha na kuimarisha uhusiano wa ujirani mwema kwa manufaa ya watu wetu, inapenda kuchukua nafasi hii tena kuitaka serikali ya Malawi kuheshimu makubaliano ya July 27 2012″ – Waziri Membe.

Pamoja na ahadi ya kuwalinda raia laki sita waliopo kwenye mwambao wa ziwa Nyasa, Waziri Membe amesema “serikali ya Tanzania inapenda kuchukua nafasi hii tena kuyaonya na kuyataka makampuni yote yanayofanya shughuli ya utafiti kwenye eneo hilo kusitisha kuanzia sasa, kuacha shughuli za utafiti katika maeneo hayo”

STORI YA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI NA DILI ALILOPATA NEW YORK.


                                      Ludovick Utoh.

Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali Ludovick Utouh amesema nafasi aliyoipata ya kuwa mjumbe wa bodi ya ukaguzi ya umoja wa mataifa haitoathiri utekelezaji wa majukumu yake ya ukaguzi ndani ya nchi.
Amesema ataendelea na majukumu yake kama kawaida na atakua akienda New York mara mbili kwa mwaka kwa muda wa miaka sita atakayokua kwenye hiyo nafasi ambapo pia watendaji 60 wa ofisi yake wameteuliwa kutekeleza majukumu ya ukaguzi kwa umoja huo wa mataifa.

EXCLUSIVE: HIZI NDIO PICHA 11 ZA UTENGENEZAJI WA VIDEO MPYA YA DOGO JANJA, YA KWANZA TOKA ATOKE TIP TOP.



                       Location ni Sayansi Kijitonyama.
















Video ya single mpya ya Dogo Janja ‘Yamoyoni’ ilikua ifanywe na Ogopa Dj’s Kenya lakini baada ya ishu flani kutokea ikabidi ifanywe na kampuni ya hapahapa Tanzania, imegharimu shilingi milioni 1.5 chini ya kundi la Watanashati linalomsimamia Dogo Janja.

Search This Blog