Friday

TAARIFA KUHUSU DHAMANA YA MWIGIZAJI LULU AMBAYO ILIKUA ITOKE LEO.


On Streets Today

Elizabeth Michael. Jana kwenye allstreetsonline.com kulikua na stori kwamba uwezekano wa mwigizaji Lulu kuachiwa kwa dhamana january 25 2013 ulikuepo.


Ni kweli ilikua iwe hivyo lakini kwa taarifa zilizotolewa na vyombo husika ni kwamba dhamana hiyo imeshindikana kutolewa leo.


Sababu kubwa ni leo kuwa sikukuu hivyo shughuli imesogezwa mbele mpaka jumatatu january 28 2013.


Mwanzoni Lulu ambae anatuhumiwa katika kesi ya mauaji bila kukusudia ilidaiwa alikua anatakiwa apate dhamana ambayo milioni 20 zilihitajika (kwa mujibu wa taarifa za ndani) ila ikashindika sababu jaji alipata udhuru.


Lulu amekua chini ya ulinzi toka kifo cha mwigizaji staa wa movie Tanzania Steven Kanumba April 2012.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.

Search This Blog