Saturday

SAFARI YA BONGO FLEVA HIYOOO KUNAKO MITAANI

  • Awa mfano wa kuigwa kwa kusaidia yatima

    • Ni wasanii wangapi wanagonga kopi za kutosha na shoo kibao lakini husahau walikotoka? Bongo Artists take this aaand ACT. 

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond, baada ya kuwa na mafanikio katika muziki wake ameanzisha mpango wa kusaidia jamii yake kama sehemu ya shukrani kutokana na mafanikio hayo, ukizingatia jamii kwa kiasi kikubwa ndiyo inayomsapoti.
hapa yeye mwenyewe (kulia) akitoa msaada wa vyakula na vitu vingine kwenye kituo cha kulea watoto yatima cha Maunga kilichopo Kinondoni Hananasif jijini Dar es Salaam.

MISS IFM 2012 KUTAKUWA NA JIPYA USIKU WA LEO??



Wakati harakati za kumsaka mrembo atakayekabidhiwa taji la Miss IFM 2012 zikiwa zinaelekea ukingoni, mashabiki na wapenzi wa industry hii ya urembo wameonekana kujawa na shauku ya kutaka kufahamu ni kipi hasa kitakuwa kipya ama cha kipekee katika mashindano haya 
 Mtanange wa kumtafuta mrembo atakeiwakilisha IFM katika mashindano ya mrembo wa vyuo vikuu unaendelea na tayari mabinti wameiva kama mnavyowaona.
 ...hapa ni maelezo kutoka kwa mwalimu kuja kwa washiriki na mpiga picha pia...
 Hapo VP?
Warembo watakaoshiriki shindano la Redds Miss IFM 2012 wakiwa kwenye pozi la picha ya pamoja kwenye mazoezi yananyika kwenye ukumbi wa Break Point Posta mpya jijini Dar Es Salaam kwenye maandalizi ya fainali itakayofanyika kwenye fukwe ya Cine Club jijini Dar Es Salaam usiku wa jumamosi ya 12/05/2012

BAADA YA KANUMBA, KIFO SASA CHAMUANDAMA JB



MCHEZA filamu anayetamba kwenye ‘game,’ Jacob Steven ‘JB’ (pichani) hivi karibuni alinusurika kuuawa na majambazi waliovamia Pub ya msanii mwenzake, Aunt Ezekiel iliyopo eneo liitwalo Gereji Mwananyamala jijini Dar.
Akizungumza na Mpekuzi wetu, JB alisema kuwa baada ya majambazi hao kuvamia katika pub hiyo saa 5.30 usiku, hakuwastukia kama walikuwa wahalifu bali alidhani ni wateja wa kawaida.


“Mimi sikuwashitukia kama wale watu walikuwa majambazi, ila baada ya kutoa bastola na kutuamuru tulale chini na tutoe kila kitu nikajua kimenuka, nikatimua mbio ambazo sijawahi kukimbia licha ya mwili wangu huu,” alisema JB.


Aliongeza kuwa, wakati akitimua mbio aliwasikia watu wakimuaru asimame lakini hakutii hadi alipofika Kituo cha daladala cha Komakoma ndipo alisimama na kumshukuru Mungu kwa kumnusuru na kifo.

Mei 7, mwaka huu usiku, majambazi kadhaa waliivamia pub ya Aunt Ezekiel na kufanikiwa kupora fedha na kumjeruhi mkononi na mgongoni kwa risasi kijana mmoja aitwaye Musa mkazi wa Sinza.

Nyeti za mwanaume zanasa ndani ya uke wa mke wa mtu Nairobi

Image of Nyeti za mwanaume zimenasa ndani ya uke wa mke wa mtu Nairobi [Video]

Wakati wa mchana katika kijiji cha TASSIA, EMBAKASI NAIROBI jamaa mmoja amekutwa akiwa AMEKWAMA yani mwili wake na umenasa na kukataa kuachiana na mwili wa MKE WA MTU walipokuwa wanajiburudisha.


JAMAA mwenyewe anadaiwa kuwa wa jamii ya WAKISII na mke wa mtu ana asili ya jamii ya WAKAMBA, ambapo inasemekana baada ya stori kuendelea sana kwamba jamaa anaiba mke wa mtu, MUME ilibidi aende kwa MGANGA kumfunga MKE WAKE ili asifanye mapenzi nje ya NDOA na akifanya hivyo ATAKWAMA, yani kukwamba wana maanisha jamaa yeyote atakae ingia kwenye mtego mwili wake hautoachana na mwili wa mwanamke huyo, itashikana na aibu iwakute

REVOLUTION TIME KWENYE GAME LA BONGO YAWADIA

Studio mpya - "DIGITAL VIBES" - kufunguliwa Morogoro maeneo ya Masika

Thursday

WANAFUNZI WANASOMA KWA KUGEUZIANA MIGONGO RUVUMA

WANAFUNZI 201 kuanzia darasa la tatu hadi la sita  katika shule ya msingi Kidugalo kata ya Rwinga wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma wanasoma katika vyumba viwili vya madarasa kwa kugeuziana migongo hali ambayo inachangia kushusha taaluma katika shule hiyo.
Wanafunzi wa darasa la tatu na la nne katika shule ya msingi Kidugalo kata ya Rwinga Namtumbo mjini mkoani Ruvuma wakisoma katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Owini Mpangala alibainisha kuwa  wanafunzi 51 wa darasa la tatu na wanafunzi 56 wa darasa la nne wanasoma katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo na wanafunzi 62 wa darasa la tano na wanafunzi 32 wa darasa la sita wanasoma katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo.
“Madarasa mawili kusomea katika chumba kimoja kunasababisha kila darasa kufundishwa vipindi vinne tu kati ya vipindi nane vinavyotakiwa kufundishwa kwa siku,walimu wawili hawawezi kuingia kwa wakati mmoja kufundisha kwenye chumba kimoja,vipindi vinne vinapotea  darasa halifundishiki’’,alisisitiza.
Kwa mujibu wa mwalimu Mpangala shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2007 yenye wanafunzi 453 ina vyumba vinne tu vya madarasa kati ya mahitaji ya vyumba nane na kwamba shule hiyo haina ofisi ya walimu hali ambayo inasababisha mwalimu mkuu na walimu kutumia ofisi moja ambayo hata hivyo haitoshi kutokana na idadi ya walimu 13 waliopo katika shule hiyo.
Kutokana na hali hiyo baadhi ya walimu wanakaa nje ya ofisi wakati wa kiangazi huku wakiendelea kufanyakazi za kusahihisha madaftari ya wanafunzi wakipigwa na jua hali ambayo inaleta kero kubwa kwa walimu na wanafunzi.
Mkuu wa shule hiyo alisema amechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na matatizo hayo ikiwa ni pamoja na kuyapeleka katika kamati ya shule na Baraza la madiwani ambayo wameahidi katika msimu ujao wa fedha wanatarajia kulipatia kipaumbele hasa kero ya upungufu wa vyumba vya madarasa,samani na ofisi ya walimu.
“Hapa kwangu uongozi wa serikali ya kijiji umekataa kujenga vibanda vya nyasi kama ilivyo katika shule nyingine kwa madai kuwa hapa ni mjini hawawezi kujenga vibanda vya nyasi ni aibu,wamefyatua tofali zipo kwenye tanuri’’,alisema.
Baadhi ya walimu wanaofundisha katika shule hiyo wamesema wanatamani kuacha kazi au kuhama katika shule hiyo kutokana na changamoto nyingi ambazo hazijapatiwa ufumbuzi kwa muda mrefu na kuchangia kushusha elimu katika shule hiyo ambayo ipo mjini.
Mratibu elimu kata ya Rwinga Thomas Komba amekiri shule za msingi katika kata yake inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo shule ya msingi Kidugalo ambapo hivi sasa uhamasishaji unafanyika ili kumaliza kero ya upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa.
Baadhi ya walimu katika shule ya msingi Kidugalo wakisahihisha madaftari ya wanafunzi nje baada ya shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2007 kukosa ofisi ya walimu

Aliongeza kuwa wananchi wa eneo la Kidugalo mwaka jana wamefyatua na kuchoma tofali kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na kwamba hivi sasa kinachosubiriwa ni nguvu toka serikalini kutoa vifaa vya kiwandani ili kuweza kufanikisha kupunguza kero hiyo ya muda mrefu.
Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo ina shule za msingi 107 kati ya hizo shule 105 zinamilikiwa na serikali na shule mbili ni za watu binafsi na mashirika ya dini.
Imeandaliwa na Albano Midelo,Namtumbo

Sunday

MASTAA 7 NDANI YA BIG BROTHER 2012.


lADY MAY (25) NAMIBIA.
PREZZO (32) KENYA.
BARBZ (34) SOUTH AFRICA.
ROCK (27) ZIMBABWE.
MAMPI (25) ZAMBIA.

DKB (26) GHANA.

GOLDIE (28) NIGERIA.photos by Global Publishers.

MIMBA YA LULU YAZUA UTATA

Utata kama Elizabeth Michael ‘Lulu’, (pichani)  ana mimba au la, umetatuliwa baada ya mwanamitindo maarufu Bongo anayefahamika kwa jina moja la Martin kutoboa siri kuwa ni kweli staa huyo ana mimba ya miezi mitatu, Risasi Jumamosi linafunguka.
Akizungumza na mwandishi wetu, Martin ambaye ni rafiki wa karibu wa Lulu anayesota rumande Segerea, Dar akiwa mshukiwa wa kwanza wa kifo cha Steven Kanumba, alisema kwa hesabu zake tangu msichana huyo aliponasa ni takribani miezi 3 sasa.
WALIJARIBU KUICHOROPOA MARA KADHAA
Jamaa huyo alifunguka kuwa baada ya Lulu kushtuka kuwa ni mjamzito alimweleza marehemu Kanumba ambapo kwa pamoja walijaribu kuichoropoa mimba hiyo lakini ikasema “sitaki” (ikashindikana).

Aliendelea kudai kuwa, baada ya mpango huo kufeli waliamua kuiacha hadi Lulu alipokumbana na dhahama ya kukaa nyuma ya nondo hadi leo.


“Yeye (Lulu) na Kanumba walijaribu mara kadhaa kuitoa lakini ikashindikana.”alisema mwanamitindo huyo.
 NDIYO CHANZO CHA ‘SHESHE’ LAO
Jamaa aliweka wazi kuwa ‘sheshe’ kubwa kati ya Lulu na marehemu Kanumba lilihusiana na mimba hiyo.
 “Kanumba alikuwa akitaka Lulu akatoe mzigo huo, lakini Kalulu Kadogo (Lulu) alikataa katakata,” alisema na kuongeza:
“Aisee ilikuwa ni ishu ya siri sana.”
TUJIKUMBUSHE
Madai ya Lulu kuwa mjamzito yaliripotiwa kwa mara ya kwanza wiki iliyopita na gazeti ndugu la hili la Amani ambapo ilielezwa kuwa mbali na kitumbo kumtoka pia, alikuwa akichagua aina ya vyakula.

KILI AWARDS YAENDELEZA SHANGWE MWANZA


Search This Blog