Saturday

MITANDAO YACHANGIA ONGEZEKO LA KASI YA UKAHABA VYUONI (UDSM) (UDOM) (CBE) (IFM)(SAUTI)


 Mitandao ya kijamii ipo inayowasaidia wanafunzi katika masomo yao na kazi, lakini wengine wanatumia mitandao hiyo visivyo. Imefahamika kuwa Baadhi ya wanafunzi wanatumia mitandao ya kijamii katika kufanikisha biashara ya ngono. PENGINE haya tunaweza kuyaweka kwenye kundi la madhara yatokanayo na utandawazi.
Uchunguzi umebaini kuwa matumizi mabaya ya teknolojia hasa mitandao ya kijamii yamechochea ongezeko la uhalifu, ubakaji, matumizi ya dawa za kulevya na zaidi biashara ya ukahaba vyuoni.
Mitandao ya ‘Facebook’, ‘Twitter’, ‘BBM’, ‘Instagram’ inafahamika kwa namna inavyoweza kuwaunganisha watu kutokana na urahisi wake katika kuitumia.
Mwananchi limebaini kuwa katika mitandao hiyo makundi mbalimbali yameanzishwa yakiwa na malengo tofauti.
Baadhi wameanzisha makundi kwa lengo la kujenga mitandao ya kibishara, kidini, michezo, burudani, vichekesho na mengine ambayo mara nyingi huwa wazi na yeyote anaweza kujiunga na kuona kinachoendelea ndani.
Mbali na hayo ndani ya mtandao wa ‘Facebook na ‘BBM’ yapo makundi yanayoendesha biashara ya ukahaba, yakiwahusisha wanafunzi wa vyuo vikuu mbalimbali nchini kwa kupitia kurasa mbalimbali kama vile ‘University Tanzania Jokes’, ‘Jicho la Mvulana Liko Fasta Kuliko Google’, ‘Benki ya Utamu Tanzania’ na nyinginezo.

Uchunguzi umebaini kuwa wanafunzi hao wanaofanya biashara ya ukahaba kwa kutumia mitandao wameweka picha na namba kwa ajili ya mawasiliano kwa mteja atakayekubaliana na bei waliyoweka.

Baadhi ya wanafunzi hao wanatumia mtandao wa ‘University Tanzania Jokes’, ‘Jicho la Mvulana Liko Fasta Kuliko Google’, ‘Benki ya Utamu Tanzania’ na nyingine katika kufanikisha biashara hiyo ya ngono.
Ukiingia katika mitandao ya Facebook, Twitter, BBM, Instagram, utabaini kuwapo kwa makundi yaliyoundwa kutengeneza mitandao ya ngono, ambayo huweka pia namba za simu za wahusika, zikiambatana na picha, ambao ikiwa utaangalia picha na kuvutiwa, unaweza ukapiga simu husika kuzungumza naye kwa kufanya mapatano kabla ya kukubaliana.

Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umebaini kuwa mwanamume anaweza kumpata msichana kutoka chuo kikuu chochote nchini anayefanya biashara ya ukahaba kupitia mitandao hiyo. 
Baadhi ya vyuo wanavyotoka wasichana wanaofanya biashara hiyo na kujitangaza kwenye mitandao ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT), Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).

Kwa nyakati tofauti, waandishi wa gazeti la Mwananchi walitembelea makundi yanayojinadi kufanya biashara hiyo pamoja na kufanya mawasiliano na wasichana watatu ambao waliweka picha na namba zao kwenye mtandao

Monday

Uhuru Kenyatta ndiye rais tajiri zaidi barani Afrika

On Streets Today

Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta ndio rais tajiri zaidi barani Afrika. Kenyatta alikamata nafasi ya 26 mwaka 2011 kwenye orodha ya watu matajiri zaidi barani Afrika kwa kuwa na utajiri unaofikia dola milioni 500.
Mtoto huyo wa rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyatta nimrithi wa mali kibao zilizopo Kenya. Anamiliki ardhi yenye ukubwa wa acre 500,000 katika maeneo mbalimbali nchini humo. Ardhi hiyo ilikuwa ya baba yake aliyoipata miaka ya 1960s na 1970s baada ya serikali ya kikoloni ya Uingereza na benki ya dunia kuwezesha maofisa wa serikali wa Kenya na matajiri kupata ardhi kutoka kwa waingereza kwa bei chee.
Uhuru na familia yake wanamiliki kampuni ya Brookside Dairies ambayo ni kubwa zaidi nchini Kenya kwa utengenezaji wa maziwa na pia ana hisa nyingi kwenye kituo cha TV cha K24 pamoja na benki moja kubwa ya biashara jijini Nairobi. Pia ana miradi mingine kibao.

PICHA ZA UCHI ZA MSANII SAPNA WA STEVE R & B ZANASWA

On Streets TodayWAKATI mabinti wengi hasa mastaa wa Bongo wakijuta baada ya picha zao za utupu walizopigwa na wapenzi wao kuvuja, kwa msanii mrembo aliyepamba video ya wimbo wa Bongo Fleva uitwao Jambojambo wa msanii Steve R&B,Aisha Firozi ‘Sapna’ ni kawaida kwani hujifotoa mwenyewe.


Chanzo makini cha Risasi kimewasilisha folda lenye picha za kutosha za mrembo huyo akiwa mtupu huku kikieleza kwamba ni mchezo wake kujipiga mwenyewe picha hizo.


Kwa sharti la kutochorwa jina lake , chanzo hicho ambacho kipo aribu na Sapna kilisema:“Yule ni mtu wangu wa karibu sana, lakini tabia yake kwa kweli huwa siipendi kabisa. Anajipiga picha chafu mwenyewe, kwake ni starehe kubwa, huwezi kuamini.”

Kikiendelea ufunguka zaidi, chanzo hicho kilipasha kuwa, picha hizo amejipiga hivi karibuni nyumbani kwa rafiki yake aitwaye Doreen, Tabata - Magengeni jijini Dar es Salaam, ambapo alikuwa akiishi naye.

KAULI YA SAPNA.....Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni; Sapna alipopigiwa simu na kuelezwa kuhusu kunaswa kwa picha hizo, kwanza alishangaa lakini akakiri kuzitambua.
“Hizo kweli ni picha zangu na nilijipiga mwenyewe sasa sijui wewe umezipataje na zimefi kaje huko kwenu? Mimi nilipiga kwa masilahi yangu mwenyewe, huwa natamani sana kujiangalia jinsi umbo langu lilivyo, ndiyo maana niliamua kujipiga na si vinginevyo.
“Kila mtu na maisha yake na mimi sikuwa na dhamira mbaya kujipiga picha hizo zaidi ya kujiangalia tu nilivyo,” alisema Sapna.

TID APEWA KICHAPO KIKALI NA MTANGAZAJI WA CLOUDS TV

On Streets Today


Mwanamuziki nyota wa Bongo flava ambaye kwa sasa amejikita kwenye muziki wa dansi, Khalid Mohammed ‘TID’, wiki iliyopita alionja joto ya jiwe baada ya kudundwa hadi kutolewa nundu puani na mtangazaji wa Clouds TV, Cedou Ayoub a.k.a Babuu.
Tukio hilo la aina yake lililotokeawiki iliyopita kwenye kiota cha burudani Bongo pale Club Maisha na kushuhudiwa na watu kibao ambapo chanzo chake kikidaiwa ni kudaiana hela.
Chanzo chetu kilimwaga umbea kuwa, siku ya tukio hilo TID alikuwa amealikwa kwenye uzinduzi wa albamu ya mwanamuziki Country Boy iliyokuwa inafanyika mjengoni humo, ambapo baada ya onesho hilo kuisha ndipo TID akiwa ‘mitungi’ alimfuata Babuu na kuanza ‘kumzingua’.
Hata hivyo, chanzo chetu kiliendelea kueleza kuwa, baada ya walinzi wa ukumbi huo kuona hali tete ya uvunjifu wa amani waliwasihi watu hao kutoka nje kabisa ya ukumbi, huku mtangazaji huyo akiwaomba walinzi hao wawaache wapimane ubavu kidogo na walipotoka nje wakaachiwa ‘ulingo’ ndipo ngumi zilianza kupigwa.
Habari zaidi toka eneo la tukio zilisema kuwa: “Watu waliwazunguka huku wakishangilia kwa muda wa dakika tano ngumi zinapigwa ndipo maabaunsa wakawaamua, lakini, tayari TID alikuwa ameshatolewa manundu kadhaa puani.”
Aidha, kwa upande wa Babuu, alipotafutwa kupitia simu yake ya kiganjani, iliita bila kupokelewa.

Hata hivyo, watu wa karibu na Babuu walilieleza gazeti hili kuwa, kufuatia TID kuchezea mkong’oto huo, kumezuka ‘bifu’ kubwa na kuna wasiwasi wa kutekana kwa mastaa hao hivyo huku Mkurugenzi wa Clouds Media, Ruge Mutahaba akitakiwa kuingilia kati suala hilo ili kuepusha balaa.

Search This Blog