Monday

Uhuru Kenyatta ndiye rais tajiri zaidi barani Afrika

On Streets Today

Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta ndio rais tajiri zaidi barani Afrika. Kenyatta alikamata nafasi ya 26 mwaka 2011 kwenye orodha ya watu matajiri zaidi barani Afrika kwa kuwa na utajiri unaofikia dola milioni 500.
Mtoto huyo wa rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyatta nimrithi wa mali kibao zilizopo Kenya. Anamiliki ardhi yenye ukubwa wa acre 500,000 katika maeneo mbalimbali nchini humo. Ardhi hiyo ilikuwa ya baba yake aliyoipata miaka ya 1960s na 1970s baada ya serikali ya kikoloni ya Uingereza na benki ya dunia kuwezesha maofisa wa serikali wa Kenya na matajiri kupata ardhi kutoka kwa waingereza kwa bei chee.
Uhuru na familia yake wanamiliki kampuni ya Brookside Dairies ambayo ni kubwa zaidi nchini Kenya kwa utengenezaji wa maziwa na pia ana hisa nyingi kwenye kituo cha TV cha K24 pamoja na benki moja kubwa ya biashara jijini Nairobi. Pia ana miradi mingine kibao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.

Search This Blog