Akizungumza
na Mpekuzi wetu, JB alisema kuwa baada ya majambazi hao kuvamia katika
pub hiyo saa 5.30 usiku, hakuwastukia kama walikuwa wahalifu bali
alidhani ni wateja wa kawaida.
“Mimi sikuwashitukia kama wale watu walikuwa majambazi, ila baada ya kutoa bastola na kutuamuru tulale chini na tutoe kila kitu nikajua kimenuka, nikatimua mbio ambazo sijawahi kukimbia licha ya mwili wangu huu,” alisema JB.
Aliongeza kuwa, wakati akitimua mbio aliwasikia watu wakimuaru asimame lakini hakutii hadi alipofika Kituo cha daladala cha Komakoma ndipo alisimama na kumshukuru Mungu kwa kumnusuru na kifo.
Mei 7, mwaka huu usiku, majambazi kadhaa waliivamia pub ya Aunt Ezekiel na kufanikiwa kupora fedha na kumjeruhi mkononi na mgongoni kwa risasi kijana mmoja aitwaye Musa mkazi wa Sinza.
“Mimi sikuwashitukia kama wale watu walikuwa majambazi, ila baada ya kutoa bastola na kutuamuru tulale chini na tutoe kila kitu nikajua kimenuka, nikatimua mbio ambazo sijawahi kukimbia licha ya mwili wangu huu,” alisema JB.
Aliongeza kuwa, wakati akitimua mbio aliwasikia watu wakimuaru asimame lakini hakutii hadi alipofika Kituo cha daladala cha Komakoma ndipo alisimama na kumshukuru Mungu kwa kumnusuru na kifo.
Mei 7, mwaka huu usiku, majambazi kadhaa waliivamia pub ya Aunt Ezekiel na kufanikiwa kupora fedha na kumjeruhi mkononi na mgongoni kwa risasi kijana mmoja aitwaye Musa mkazi wa Sinza.
No comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.