Sunday

KILI AWARDS YAENDELEZA SHANGWE MWANZA


Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Kilimanaro Premium Lager ambao ni wadhamini wakuu wa Kilimanjaro Music Awards hivi karibuni wamezindua rasmi ziara ya washindi wa tuzo hizi kwa mwaka 2012.
Ziara hizi zitakazofanyika katika mikoa 6 ya Tanzânia zitahusisha uvumbuzi wa vipaji vichanga vya wasanii wa muziki wa kizazi kipya. Mikoa itakayohusishwa ni Dodoma, Kilimanjaro, Mbeya, Mtwara pamoja na Mwanza na kilele kuwa Dar es Salaam.
Kama alivyokaririwa meneja masoko wa bia hiyo, lengo kuu la ziara hii ni kuwapa nafasi wasanii chipukizi kushiriki kikamilifu na kuonyesha vipaji vyao kama mpango wa bia ya Kilimanjaro wa kuzindua vipaji unavyosema.
“Tunataka kuondoa mawazo hasi yaliyopo kwamba Tuzo za muziki za Kili ni za Dar es Salaam tu. Mwaka huu licha ya kuwapeleka washindi wa tuzo mikoani tumeamua pia kuzindua vipaji vipya kweye mikoa hiyo kwani tunaamini kuwa vipaji vya muziki vinapatikana Tanzânia nzima. Vilevile tutawapa nafasi wasaniii watakaovumbuliwa kuimba na washindi vinara wa tuzo za Kili ambapo mshindi mmoja wa kila mkoa ataletwa Dar es Salaam kushiriki kwenye tamasha la mwisho la ziara, na pia kurekodiwa nyimbo moja ya kumwezesha kuanza safari yake ya muziki.” Alisema George Kavishe meneja masoko wa  bia ya Kilimanjaro.

Kwa mkoa wa mwanza ziara hii ilianza kwa kutafuta vipaji vya wasanii chipukizi ambayo ilifanyika tarehe 29 Aprili ambapo majaji walikuwa ni pamoja na Juma Nature, Proffessor Jay na Queen Darleen. 

Jana tarehe 5 may  KILI AWARDS WINNERS ILIKUWA NAMNA HII.........





 Show ya hapa Mwanza ilifunguliwa na msanii wa taarabu Isha Mashauzi, shangwe zilikuwa zakutosha kabisa na wapenzi wa burudani ya taarabu walipata chakula cha ubongo.


Mashabiki kibao 
 
 Akafuatia msanii aliyechukuwa tuzo ya RnB anajulikana kama Ben Pol
 Misago, Hellen & Dullah
Barnaba, Hellen & Sam Misago 
Kaka mkubwa ndio aliyekuwa akiangalia ulinzi wa wasanii wote wakiwa salama 

 Wacheza show wa msanii Diamond
 Ikafika zamu ya mtoto wa Zanzibar AT kupanda kwa steji
 Ikafika zamu ya msanii mwenye tuzo 3 kupanda kwa steji, hapa namzungumzia Diamond 
 Mtoto wa Tanga Roma ndio aliyefunga show kwa upande huu wa Mwanza.Kwa mapicha zaidi ingia hapa BONGO STAR LINK- DJ CHOKA


KATIKA HARAKATI ZA KUSAKA CHIPUKIZI BOMBA HUKO ROCK CITY ILIKWENDAGA POA KIHIVI........................
washiriki kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mwanzawaliojitokeza kwa ajili ya shindano hili na hapa walikuwa wakiendelea kusubiri kuitwa kwa ajili ya usaili

 Jaji wa kusaka vipaji vya wasanii wachanga mkoani Mwanza katika ziara ya washindi wa tuzo za KILI 2012 (Juma Nature- wa pili kushoto) akitoa maelekezo kwa washiriki waliohudhuria kwenye tamasha hilo lililofanyika katika ukumbi wa  VILLA PARK jijini Mwanza. kutoka kulia ni Profesa J, Queen Darleen, Nature na Henry Mdimu.





 Henry Mdimu akitema cheche kwa vijana chipukizi waliokuwa wamejazana Villa tayari kwa tamasha.


Joseph Haule naye hakubaki nyuma, alifunguka kiume kuwasihi ma-underground wakomae kisabuni na kuwaasa waache uoga bali wafanye kilichotakiwa kufanyika.

 Hapa ni baadhi ya washiriki wakionesha manjonjo steji huku wakishuhudiwa vyema na majaji wao..


kazi na dawa ndo mtindo wa kisasa..msosi kama kawa. Hapa ni jopo zima la wasaka vipaji wakipata kipooza koo wakati wa mapumziko kabla ya kurudi kwa raundi ya pili








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.

Search This Blog