Sunday

MIMBA YA LULU YAZUA UTATA

Utata kama Elizabeth Michael ‘Lulu’, (pichani)  ana mimba au la, umetatuliwa baada ya mwanamitindo maarufu Bongo anayefahamika kwa jina moja la Martin kutoboa siri kuwa ni kweli staa huyo ana mimba ya miezi mitatu, Risasi Jumamosi linafunguka.
Akizungumza na mwandishi wetu, Martin ambaye ni rafiki wa karibu wa Lulu anayesota rumande Segerea, Dar akiwa mshukiwa wa kwanza wa kifo cha Steven Kanumba, alisema kwa hesabu zake tangu msichana huyo aliponasa ni takribani miezi 3 sasa.
WALIJARIBU KUICHOROPOA MARA KADHAA
Jamaa huyo alifunguka kuwa baada ya Lulu kushtuka kuwa ni mjamzito alimweleza marehemu Kanumba ambapo kwa pamoja walijaribu kuichoropoa mimba hiyo lakini ikasema “sitaki” (ikashindikana).

Aliendelea kudai kuwa, baada ya mpango huo kufeli waliamua kuiacha hadi Lulu alipokumbana na dhahama ya kukaa nyuma ya nondo hadi leo.


“Yeye (Lulu) na Kanumba walijaribu mara kadhaa kuitoa lakini ikashindikana.”alisema mwanamitindo huyo.
 NDIYO CHANZO CHA ‘SHESHE’ LAO
Jamaa aliweka wazi kuwa ‘sheshe’ kubwa kati ya Lulu na marehemu Kanumba lilihusiana na mimba hiyo.
 “Kanumba alikuwa akitaka Lulu akatoe mzigo huo, lakini Kalulu Kadogo (Lulu) alikataa katakata,” alisema na kuongeza:
“Aisee ilikuwa ni ishu ya siri sana.”
TUJIKUMBUSHE
Madai ya Lulu kuwa mjamzito yaliripotiwa kwa mara ya kwanza wiki iliyopita na gazeti ndugu la hili la Amani ambapo ilielezwa kuwa mbali na kitumbo kumtoka pia, alikuwa akichagua aina ya vyakula.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.

Search This Blog