On Streets Today
Naibu Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Amos Makalla |
Makalla ambaye ni Mbunge wa Jimbo hilo amekabidhi hundi za Sh. milioni 5 kwa kila kata ili kuwezesha kuanza kwa mchakato wa ujenzi wa masoko ya kisasa katika maeneo yaliyotengwa wakati wa ziara yake ya kukagua na kuhimiza maendeleo kwa wananchi wa wilaya hiyo.
Mbunge huyo alitaka mpango wa ujenzi wa masoko hayo uanze kufanyika mara moja ikiwa na kuweka makadiriko ya gharama za ujenzi.
Kata ya Mvomero ilikuwa ya kwanza kukabidhiwa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika hivi karibuni na pia kuuagiza uongozi wake kuanza mchakato wa ujenzi wa soko la kisasa litakaotumiwa na wananchi wa ndani na nje ya kata ili kwenda na kasi ya ukuaji wa mji huo.
Aliwataka wananchi kwa kushirikianana uongozi wao na nguvu za Mbunge atakapofikisha hatua nzuri ya ujenzi itakuwa ni rahisi kuwashawishi wadau wengine kuchangia ujenzi huo pamoja na Halmashauri ya Wilaya kutenga bajeti ya fedha za kuendeleza ujenzi huo.
“ Huu ni mkakati wangu na ni miongoni mwa kero zilizotolewa na wananchi juu ya ukosefu wa masoko “ alisema Mbunge huyo .
Mbunge huyo alitoa hundi za kiwango kama hicho kwa viongozi wa Serikali ya Kata ya Kibati, Dakawa na Mlali na kusema masoko hayo yakikamilishwa yatawanufaisha wakulima na wananchi katika mifumo mizuri ya bei ya mazao .
Hata hivyo aliwaonya Viongozi wa Serikali za Vijiji na Kata hizo ,kuwa fedha hizo zisitumiwe katika shughuli nyingine kinyume na ilivyokusudiwa na viongozi watakaokiuka utaratibu watawajibishwa.
No comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.