Yapo mambo ambayo hata unapotaka kuyakalia kimya tu inakuwa shida
kidogo.Juzi,Shirika La Ndege Tanzania(ATC) limepata ndege mbadala(nasema
mbadala badala ya mpya kwa makusudi).Ndege hii imekodishwa...Je ni kweli kuwa Uwezo wa
kununua bado hatuna?.Cha kusikitisha zaidi ni kwamba tunavishana mataji kujipongeza kwa kufanikiwa kukodi ndege moja ya abiria!!!!????
Pamoja na hayo,kwetu sisi yaelekea kuwa na ndege ya kukodisha ni mafanikio makubwa sana.Yanastahili makofi,vigelegele na keki.Kweli??
Pamoja na hayo,kwetu sisi yaelekea kuwa na ndege ya kukodisha ni mafanikio makubwa sana.Yanastahili makofi,vigelegele na keki.Kweli??
Wafanyakazi
wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakishuka katika ndege mpya aina
ya Boeing 737-500 iliyokodishwa na shirika hilo yenye uwezo wa kubeba
abiria 108. Ndege hiyo itaanza kuruka baada ya wiki moja.
Kaimu
Mkurugenzi na Mwenyekiti Mtendaji wa Shirika la Ndege la Tanzania
(ATCL) Paul Chizi akiongea na waandishi wa habari mara bada ya kuwasili
kwa ndege mpya aina ya Boeing 737-500 iliyokodishwa na shirika hilo
yenye uwezo wa kubeba abiria 108.
Wafanyakazi
wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakikata keki kusherekea ujio wa
ndege ndege mpya aina ya Boeing 737-500. Wapili kushoto ni Kaimu
Mkurugenzi na Mwenyekiti Mtendaji wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL )
Paul Chizi
GOD SAVE US!
Picha na maelezo ya picha kwa hisani ya G.Sengo
No comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.